Saed Kubenea
Taarifa hiyo imetolewa hii leo Septemba 11, 2020, na Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma wa chama hicho, Janeth Rithe, muda mfupi tu tangu mgombea Ubunge huyo kupata dhamana baada ya kukamilisha taratibu zote za kisheria katika kesi inayomkabili.
Taarifa hiyo pia imewapongeza mawakili waliofanikisha hatua ya Kubenea kupata dhamana hiyo, huku wakiwasihi wanachama wa chama hicho kufuatilia ratiba ya mikutano ya kampeni ili waweze kusikiliza sera na ahadi zilizomo kwenye ilani ya chama hicho.
"Aidha Ndugu Saed Kubenea, anatarajia kuzungumza na vyombo vya habari katika siku za hivi karibuni juu ya suala hili", imeeleza taarifa hiyo.