Alhamisi , 29th Dec , 2022

Benjamin Netanyahu ataapishwa leo kama Waziri Mkuu wa Israel kwa mara ya sita na kufanya kiongozi huyo kuweka rekodi ya kiongozi aliyerejea madarakani mara nyingi nchini humo

Serikali mpya ya Netanyahu inatarajiwa kuapishwa mjini Jerusalem ikiwa ni miezi miwili baada ya waziri mkuu huyo mteule kushinda uchaguzi wa bunge nchini humo

Hii ni serikali ya siasa za mrengo wa kulia zaidi ambayo Israeli imewahi kuwa nayo, huku wanasiasa wa siasa kali za mrengo huo pia wakijumuishwa kwa mara ya kwanza katika serikali ya mseto