Alhamisi , 9th Jun , 2022

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, ameendelea kukemea na kulaani vitendo vya mauaji vinavyotokana na wivu wa mapenzi ambavyo vimekuwa vikitekelezwa na baadhi ya watu kwenye jamii jambo ambalo ni kinyume na sheria za nchi.

IGP Sirro, wakati akizungumza na wakazi wa Migori Iringa

IGP Sirro amesema hayo akiwa eneo la Migori mkoani Iringa wakati akizungumza na wananchi wa eneo hilo.

"Umemuoa mwanamke wako au hawara yako mnaishi pamoja, mkahitilafiana kuna sababu ya kutafuta visu unamchoma mwenzako unamuua, ebu Watanzania tufike mahala tubadilike huu ni ujinga, kama amekuzengua si unaachane naye, kwahiyo shida tunayopata sasa hivi mauaji mengi ni hayo hayo (Mapenzi)", amesema IGP Sirro

Aidha IGP Sirro ameongeza "Lakini akina dada pia uangalie na mwanaume gani unakaa naye, sio kila mwanaume ni bora kuna wanaume wengine mizigo, na kuna wanawake wengine mizigo si ndio eeh,".