Jumatano , 12th Dec , 2018

Kesi ya kusambaza picha za utupu inayomkabili Miss Tanzania 2016, Wema Sepetu imetajwa leo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam.

Wema Sepetu akiwa mahakamani

Kwa mujibu mahakama kesi hiyo imelezimika kusogezwa mbele hadi januari 28 mwakani kwa ajili ya kuanza kusikilizwa tena.

Miongoni mwa sababu zilizopelekea kesi hiyo kuhairishwa ni upande wa Jamhuri kudai upelelezi haujamilika hivyo wameiomba mahakama kuipangia tena tarehe nyingine kesi hiyo ili ikamilishe kazi ya kupata ushahidi.

Msanii Wema Sepetu anashtakiwa kwa kosa la kusambaza picha za faragha mtandaoni hali iliyopelekea kuzua taharuki kwenye jamii ambapo pia ni kinyume wa mujibu wa sheria za nchi.

Kwa mara ya kwanza Msanii huyo alifikishwa mahakamani novemba 21 kwa shauri la kesi hiyo lilitajwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya hakimu, Maira Kasonde huku Wakili wa utetezi akiwa Ruben Simwanza na upande wa Jamhuri ukisimamiwa na Wakili Jenifer Masue.

Jana Mahakama ilitangaza kwenda likizo ya mwisho wa mwaka ambayo itaanza novemba 15 hadi Januari 28, 2019.