
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro
IGP Sirro amesema hayo leo wakati akizindua kitabu cha muongozo wa kufichua na kuzuia uhalifu ,kitabu ambacho kinalenga kutoa dira hasa katika utekelezaji wa mpango wa Polisi kupitia mpango mkakati wa ushirikishwaji wa jamii.
“Nitoe angalizo kuna baadhi ya wahalifu wametoka magereza siku za karibuni ambao baada ya vifungo vyao wamesamehewe na Mhe. Rais, kuna baadhi ya matukio ambayo kwetu tulikuwa tumeanza kuyasahau yameanza kurudi tena kwa nguvu kubwa, niwaombe hao ambao hawataki kubadilika, kama hutaki kubadilika na familia yako imeshindwa kukubadilisha au jamii usijelaumu serikali,” amesema IGP Sirro
Aidha IGP Sirro amewaomba watanzania kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kuhusiana na vitendo vya uhalifu ,huku akiwaonya wale wanaojikita katika kutelekeza matukio ya uhalifu kuwa jeshi la polisi halitokaa pembeni bali litatekeleza wajibu wake.