
Na aliyekuwa Mkuu wa Kikosi hicho Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Wilbroad Mtafungwa ameteuliwa kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza
Aidha IGP Wambura amempangia Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei, kuwa Mkuu wa Kitengo cha Polisi Wasaidizi na Kampuni Binafsi za Ulinzi nchini ambapo anachukuwa nafasi ya Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Issack Katamiti.
Katika Uteuzi huo aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkoa wa Kipolisi Rufiji Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Protus Mutayoba, amekuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rufiji baada ya Kamanda wa Mkoa huo kuhamishiwa Mkoa wa Kipolisi Temeke hivi karibuni.