Jumanne , 7th Jun , 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 07 Juni, 2016 amemteua Jaji Ferdinand Leons Katipwa Wambali kuwa Jaji Kiongozi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 07 Juni, 2016 amemteua Jaji Ferdinand Leons Katipwa Wambali kuwa Jaji Kiongozi.

Jaji Ferdinand Leons Katipwa Wambali anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Shaaban Ally Lila aliyeteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.

Kabla ya uteuzi huo, Jaji Ferdinand Leons Katipwa Wambali alikuwa Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto, Mkoani Tanga.Uteuzi huu unaanza mara moja.