Jumatatu , 27th Jan , 2020

Rais wa Dkt. John Pombe Magufuli amemtaka Waziri Mambo ya Ndani ya Nchi Simbachawene kutumia mbinu bora katika kuiongoza Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kama ambavyo anafanya Waziri wa Ulinzi Hussein Mwinyi.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo wakati akiwaapisha Mawaziri wawili na Mbalozi watatu Ikulu jijini Dar es salaam.

Rais Magufuli amemueleza Simbachawene kuwa "Waziri wa Mambo ya Ndani ina namna yake ya kuviendesha, ndiyo maana Waziri Mwinyi amekaa sana wizara ya Ulinzi, huwezi akakaa mbele ukakuta Mwinyi amewatukana Mabrigedia, katumie hizo mbinu kuongoza ndiyo maana unaona wakuu wa Vyombo vya ulinzi na usalama wanakuja kuripoti kwangu moja kwa moja"

"Unaenda kwenye Wizara ambayo nafikiri ina Mapepo naomba hayo mapepo yasikuingie, kawe mkali kasimamie na mimi najua utaweza" ameongeza Rais Magufuli