
Mwajiri wa marehemu ambaye alishiriki maziko ya ndugu huyo, amesema marehemu Jamal Mkumbo alizikwa Desemba 25, mwaka 2018 kwa kufuata tararibu zote lakini ameshangazwa kukuta kaburi limefukuliwa na sanda kuchomwa moto kutokana nakudaiwa kuwa inawezekana ni imani za kishirikina.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kitongoji hicho bw. Jackson Job amekiri kutokea kwa tukio hilo na wamekemea tabia za aina hiyo.
Matukio ya makaburi kufukuliwa wilayani Manyoni yamekuwa yakitokea mara kwa mara na kudaiwa wanaofanya hivyo wamekuwa wakijihusisha na imani za kishirikina.