Alhamisi , 1st Sep , 2022

Kasino iliyopo Mwanza  Hotel  jijini Mwanza imeteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo huku chanzo cha moto huo kikiwa bado hakijafahamika

Inaelezwea kuwa hakuna hakuna mtu aliyedhurika na moto huo  japo umesababisha hasara katika kasino hiyo kwa kuteketeza vitu vyote vilivyokuwa ndani

Jeshi la zimamoto na uokoaji lilifika kwa wakati na kuanza kuuzima moto huo ili usiendelee kuleta madhara kufuatia hoteli hiyo kuwa katikati ya jiji la Mwanza na kuzungukwa na majengo mengine 

Miongoni mwa waliofika katika tukio hilo ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza Adam Malima 

Kaimu kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji Kamila Labani amesema wamefanikiwa kuudhibiti moto huo usisambae katika hoteli hiyo huku bado wanaendelea kuchunguza chanzo cha moto huo