Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Arusha SP Solomon Mwangamilo
SP Mwangamilo, amewataka pia madereva hao kuacha visingizio hivyo, badala yake wawe washauri wazuri kwa mabosi zao kwa kuwaambia ukweli kwamba endapo wakiendesha kwa kasi kubwa wanaweza kusababisha ajali.
"Wewe ni mshauri wa kiongozi, mshauri kwa hekima kwamba barabara hii sio rafiki kama tukienda kwa kasi tunaweza kupata ajali, overspeeding ni jambo ambalo unaweza kuli-manage, nasema tuache visingizo kwamba nililazimishwa," amesema SP Mwangamilo



