mamlaka za afya nchini humo zimethibitisha kifo hicho,ambapo msichana huyo kutoka jimbo la Prey Veng vijijini alipatikana na virusi vya H5N1 siku ya Jumatano.
Taarifa zinasema msichana huyo alikuwa ameugua kwa wiki moja ambapo alipatwa na homa kali, kikohozi na maumivu ya koo.
Wizara ya afya ya Cambodia imesema baba yake pia alipimwa na wengine 11 wamepimwa.
Hii leo , Waziri wa Afya Mam Bunheng amesema ni maambukizi ya kwanza ya binadamu yanayojulikana ya aina ya H5N1 nchini Cambodia tangu 2014.Msichana huyo alikuwa amechukuliwa kutoka kijijini kwake hadi hospitali ya watoto katika mji mkuu Phnom Penh lakini alifariki muda mfupi baada ya kugundulika.




