Mkuu wa Mkoa Dar es salaam Paul Makonda
Paul Makonda ametoa kauli hiyo jijini Dar es salaam ambapo amesema nia yake kama Mkuu wa Mkoa ni kuhakikisha wananchi wa Mkoa wake wakiwemo wanaume na wanawake wanapima ugonjwa tezi dume.
Makonda amesema, "nadhani mwaka huu ndiyo sahihi wa kuendesha zoezi la upimaji wa tezi dume, nataka wanaume na wanawake wote tunaenda uchaguzi wa 2019, 2020 hakuna tezi dume."
"Kama wewe ni mwananchi wa Dar es salaam na unaelekea Dodoma tutakufuata huko hatutaki uende mkoa mwingine ukiwa unaumwa, niwaombe wananchi wa Dar es salaam wajitokeze kupima na usipokuja tutakufuata nyumbani kwa sababu ni jukumu letu kukulinda", ameongeza Makonda.