Jumatatu , 20th Jul , 2015

Serikali mkoani Mbeya imeyataka mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kuweka wazi takwimu za mafanikio ya miradi ya maendeleo yanayoendeshwa katika ili kukabiliana na umasikini nchini Tanzania

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro

Akizungumza Wilayani Momba Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro amesema hatua hiyo itasaidia kufahamu mafanikio tangu kuanzishwa kwa mashirika hayo kiasi cha fedha kilichotumika katika utekelezaji miradi na jinsi umasikini ulivyopungua katika jamii.

Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa Programu za maendeleo ya wasambazaji wa pembejeo za kilimo ADP, Wilayani Mbozi, Victor Elimshau amesema mradi huo utafanya kazi katika wilaya za Ileje, Mbozi na Momba.

Elimshau amesema lengo la mradi huo ni kuongeza uwezo wa huduma za fedha kwa wakulima wadogo wadogo ili waweze kupata pembejeo za kilimo.