 
 
Lengo  la  kukutana  kwa viongozi  hao  ni  kushuhudia  utiaji  saini  wa  makubaliano  ya  mazungumzo  yaliyokuwa  yanaendelea  kwa   usimamizi  na  uratibu  wa  chama cha  mapinduzi  chini  ya  uenyekiti  wa makamu  mwenyekiti  mstaafu  wa  CCM  mzee John  Malechele.
Baada ya mazungumzao hayo kuanza mwezi Oktoba mwaka jana viongozi wa chama tawala cha (SPLM) ambacho kimegawanyika makundi matatu moja likiwa kundi lililoko madarakani chini ya Rais Salva Kiir.
Kundi la pili linaloongozwa na aliyekuwa makamu wa Rais Dkt Rieck Machar na la Tatu ni lile la waliokuwa wafungwa wa kisiasa wamekutana mara kadhaa jiji Arusha ambapo walikubaliana kusaini mkataba wa kumaliza mgogoro huo, zoezi ambalo hadi muda huu halijafanyika na mazungumzo yanaendelea.
Viongozi waliiwasili jijini Arusha kwa lengo la kushuhudia utiaji sahihi huo ni pamoja marais Dkt Jakaya Kikwete wa Tanzania, Uhuru Kenyata wa Kenya na Yoweri Museven wa Uganda.
Wengine ni pamoja na Makamu wa Rais Tanzania Dkt Mohamed Gharibu Bilal , Makamu wa Rais wa Afrika Kusini Sirili Ramafosa, na mawaziri na watendaji wa sekta mbalimbali.

 
 

 
 
 
 
 
