
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara kata ya Mkumbara wilaya ya Korogwe Malima amesema viongozi wa makundi hayo ya Tembo watavishwa kola ili wafahamike mahali walipo kama njia ya kudhibitiwa kurejea kwenywe makazi ya watu.
Wataalamu wa wanyamapori kutoka hifadhi ya Taifa ya Saadan na Taasisi ya Utafiti wa Wanyama Pori TAWIRI, wamesema baada ya kuibuka kwa tembo hao jitihada mbalimbali zimeanza kufanyika.
Maeneo yanayovamiwa na tembo hao ni kata ya Mkumbara, kata ya Mkomazi wilayani Korogwe, kata ya Mnazi na kata ya Lunguza wilayani Lushoto, na wanadaiwa kutokea hifadhi ya Mkomazi iliyopo mkoani kilimanjaro.