
Makabidhiano ya mradi huo yamefanyika katika ofisi ya TANESCO kanda ya magharibi Mkoani Tabora ambapo meneja uthibiti na ufatiliaji mhandisi Yusufu Ismail amesema mradi huo utatekelezwa kwa muda wa miezi 18 na utawafikia zaidi ya wananchi 2000
Awali mkandarasi wa mradi huo akitambulishwa katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Tabora, balozi Dkt. Batilda Buriani amemtaka kuhakikisha anatoa kipaumbele cha nafasi za ajira kwa wakazi wa Tabora pamoja na kuwapa malipo kwa wakati
Mradi huo wa kufikisha huduma ya umeme pembezoni mwa miji (PERI URBAN) unatekelezwa chini ya mkandarasi wa ndani kupitia kampuni ya OK ELETRICAL SERVICES LTD