Jumanne , 20th Feb , 2018

Mtumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Hassan Abuutwalib maarufu Kiringo anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 13.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharib Unguja, Hassan Nassir Ali amesema wamemkamata jana (Jumatatu) katika maeneo ya uwanja wa ndege Zanzibar alipokuwa akijaribu kuondoka kuelekea Mwanza.

"Mlalamikaje ambaye mwenye miaka 54 jina lake nalihifadhi alikuja kutoa malalamiko kuwa mtoto wake alichukuliwa na Kiringi na kumpeleka katika nyumba iliyokuwa haijamalizwa kujengwa huko Fuoni uwandani ambapo inadaiwa alifanikiwa kumlawiti baada ya kumpa dawa za kupoteza fahamu na kumsababishia maumivu sehemu zake za siri za nyuma", amesema Kamanda Nassir.

Aidha, Kamanda Nassir amesema uchunguzi wa madaktari ulithibitisha kuathirika sehemu za siri za nyuma za mtoto huyo

Kwa upande mwingine, Kamanda Nassir amesema ameunda timu ya uchunguzi iliyojumuisha wakuu wa upelelezi wa wilaya tatu wilaya ya mjini, wilaya ya Magharibi A na B ili wakachunguze ukweli wa tukio zima lilotokea.