
Kamba ya katani
Karani huyo aliyefahamika kwa jina la Edmund Zakayo, amejinyonga Agosti 22, 2022, majira ya saa 10:00 ndani kwake kwa kujitundika juu ya kenchi ya nyumba kwa kutumia kamba ya katani iliyosokotwa .
Katika eneo la tukio hilo jeshi la polisi lilikuta ujumbe ambao uliandikwa na marehemu ukihusisha mgogoro wa kifamilia baina yake na mke wake, hata hivyo pamoja na barua hiyo marehemu aliacha nyaraka zote ambazo alikabidhiwa kama karani kwa ajili ya zoezi la sensa ikiwemo kishikwambi.