Jumapili , 23rd Oct , 2022

Mwili wa mtaalamu wa maabara aliyetoweka wiki iliyopita umepatikana katika mto Baratorn, Kiminini nchini Kenya.

Marehemu Judith Nafula Konya

Marehemu Judith Nafula Konya  (50) alitoweka Oktoba 18 mwaka huu , jambo ambalo liliwashangaza waumini wenzake , maana ilikua sio rahisi yeye binafsi kutoweka bila kusema alipo.

Mtoto wake  wa kiume mwenye umri wa miaka 22 Brian Wafula ambaye anasemekana kumtishia kumuua baada ya kutofautiana kuhusu wizi wa mazao ya shambani , alitoweka katika kipindi ambacho mama yake alikua hajulikani alipo.

Vyombo vya haabri nchini Kenya vinaripoti kwamba mwili wake ulikutwa jumamosi ya jana , baada ya mtoto mmoja kusema kwamba ameona mwili ukielea mtoni .

Polisi wanamtafuta mtoto wake ambaye ametoweka baad aya tukio hilo, na kwamba mtoto huyo anasemekana kuwa na uraibu wa matumizi ya dawa za kulevya.