Alhamisi , 16th Dec , 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan amesema ataigawa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee Watoto ili ibaki kuwa Wizara ya Afya wakati nyingine ikibaki kuhusika na masuala mengine Jamii Jinsia Wazee Watoto.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan

Rais Samia ameyasema hayo leo Desemba 16, 2021, kwenye Uzinduzi wa Kamati ya Ushauri ya Kitaifa kuhusu Utekelezaji wa Ahadi za Nchi Kwenye Jukwaa la Kizazi chenye Usawa katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

"Wizara hizi mbili mkizitizama ni afya na na na na.., maamuuzi yangu ni kuitenga wizara itakayoshughulikia jinsi maendeleo ya wanawake na mambo mengine kutoka kwenye kuchanganywa na Wizara Ya Afya," amesema Rais Samia Suluhu.

Zaidi Tazama Video hapo chini akieleza