Ijumaa , 25th Feb , 2022

Wizara ya Mambo ya Nje imesema kuwa hadi sasa hakuna Mtanzania aliyepata madhara yoyote kufuatia hali inayoendelea nchini Ukraine, na kuwataka waendelee kuwa watulivu wakati serikali ikiendelea kufuatilia usalama wao kwa kushirikiana na mamlaka mbalimbali za Ukraine.

Bendera ya nchi ya Ukraine

Taarifa hiyo imetolewa hii leo Februari 25, 2022, na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano serikalini wa Wizara hiyo, Emmanuel Buhohela, na kwamba serikali pia imewashauri Watanzania walioko huko kufuata maelekezo yote yanayotolewa na Ukraine, pamoja na kuendelea kuwasiliana na Ubalozi wa nchini Sweden ambao unaiwakilisha Ukraine kwa jambo lolote la dharura.