
Mashambulizi haya ya asubuhi yalitekelezwa wakati Kyiv inajiandaa kufanya mashambulizi ya kujaribu kulirejesha tena eneo lililokaliwa na Urusi.
Katika jiji la kati la Uman, wazima moto walipambana na moto mkali katika jengo la makazi ambalo lilikuwa limeshambuliwa kwenye ghorofa ya juu. Takriban watu 10 waliuawa, wakiwemo watoto wawili, na tisa walipelekwa hospitalini, gavana wa mkoa Ihor Taburets alisema.
Mwanaume mtu mzima aliyevalia barakoa aliliakwa uchungu, na mwanamke akaja kumliwaza. "Mwanzoni madirisha yalilipuliwa, kisha mlipuko mkubwa ukatokea," mkazi wa jengo hilo la ghorofa ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Olga alisema wakati waokoaji wakiendelea kufukua vifusi. "Kila kitu kilirushwa nje."