Jumatatu , 12th Dec , 2022

Katibu tawala msaidizi sekta ya uchumi na uzalishaji mkoani Mwanza Emily Kasagala amezitaka shule mbalimbali zikiwemo za dini kujiepusha na wizi wa mitihani ambao umekithiri kwa baadhi ya shule nchini na kuziasa kufundisha wa weledi ikiwemo na kuzingatia maadili mema

Katibu tawala msaidizi sekta ya uchumi na uzalishaji mkoani Mwanza Emily Kasagala

Kauli hiyo ameitoa wakati akiweka wakfu jengo la bweni la wavulana katika kituo cha kusaidia watoto wenye mahitaji maalum kilichopo eneo la Nyasaka Manispaa ya Ilemela sambasamba na maadhimisho ya miaka 25 ya huduma ya kituo hicho.

" Na kujiepusha na vitendo vibovu vya wizi wa mitihani kama ambavyo tumesikia mwaka huu baadhi ya shule zimefutiwa matokeo kwa sababu ya mashindano kwamba shule yangu iwe bora sasa matokeo yake ni kwamba tunaandaa wataalamu ambao hawana taaluma ya kutosha matokeo yake tunakuwa na madaktari ambao siyo madaktari kamili" amesema Kasagala