Jumatano , 4th Dec , 2019

Waziri Mkuu mstaafu Fredrick Sumaye leo Desemba 4, 2019 ametangaza kuondoka CHADEMA.

Waziri Mkuu mstaafu Fredrick Sumaye

Akiongea leo kwenye mkutano wake na waandishi wa Habari, Sumaye amesema ameamua kufanya hivyo kutokana na figisu alizofanyiwa baada ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Chama Taifa.

Ameeleza kuwa alitaka kugombea nafasi ya Uenyekiti ili kuondoa dhana iliyopo miongoni mwa watu kua nafasi ya Mwenyekiti ndani ya CHADEMA ni ya Freeman Mbowe na haiguswi.
 

 

Pia ametaja sababu za kusitisha nia ya kugombea Uenyekiti wa Chama Taifa. 'Nasitisha rasmi safari hiyo kwa usalama wangu, usalama wa wanachama na chama chenyewe, maana Mwenyekiti Mbowe ameshasema sumu haionjwi kwa ulimi na mimi sitaki kuionja kwa sumu hiyo' - Fredrick Sumaye.

Tazama Video hapo chini akiongea.