Jumatano , 4th Dec , 2019

Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye, anatarajiwa kuzungumza na vyombo vya habari leo, jijini Dar es salaam kuhusiana na suala la uchaguzi unaoendelea ndani ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi yake imeeleza kwamba Sumaye, atazungumza na vyombo vya habari majira ya saa 5:00 kamili asubuhi, katika jengo la LAPF Tower, lililopo Makumbusho jijini Dar es salaam.

Hivi karibuni katika uchaguzi wa ndani wa chama hicho Fredrick Sumaye, alishindwa kwenye uchaguzi wa ndani wakati akigombea nafasi ya Uenyekiti wa Kanda ya Pwani, ambapo alipigiwa kura za ndiyo 28 na hapana 44.

Hivi karibuni akizungumza na EATV na EA Radio Digital kabla ya kufanyika kwa uchaguzi huo, Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye alisema kuwa,

"Kwa sasa siwezi kuwaambia chochote nitaenda kuwaambia hukohuko ndani, ila nikishapita naombeni mnitafute ndiyo nije, lakini kwa sasa siwezi kusema chochote kwa sababu nikifanya hivyo nitakuwa nimefanya tambo za kampeni ambazo mimi sitaki kufanya".