Jumanne , 31st Aug , 2021

Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, linaendelea kunzia leo Agosti 31, 2021 ambapo Mkutano wa nne Kikao cha Kwanza unafanyika katika ukumbi wa bunge jijini Dodoma.

Mbunge wa Ukonga Jerry Slaa (kushoto) na Mbunge wa Kawe Josephat Gwajima (kulia)

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na bunge kutakuwa na maswali na majibu kwa wizara mbalimbali ikiwemo ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Wizara ya Mambo ya ndani ya Nchi.

Mbali na ratiba hiyo pia Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itawasilisha taarifa yake. 

Kamati hiyo iliwahoji wabunge mbalimbali ikianza Agosti 24 na 25, 2021 kwa mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima na Agosti 26 ikamhoji Mbunge wa Ukonga, Jerry Slaa.

Tazama video hapo chini mkutano ukiendelea.