Ijumaa , 16th Apr , 2021

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Mary Masanja amesema kuhusu suala la fidia kwa vijiji vilivyovamiwa na tembo wamekuwa na utaratibu wa kufanya uthamini pale changamoto hiyo inapotokea na kisha hulipa fidia wananchi kulingana na athari ilivyojitokeza.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Mary Masanja

Mhe.Mary amesema hayo akijibu swali la Mbunge wa Mbarali Francis Mtega aliyeuliza juu ya lini serikali italipa fidia kwa wananchi wa vijiji vitano vya Kata ya Iguva vilivyovamiwa na makundi makubwa ya tembo nakuharibu mazao yao yote hivyo kuwaweka hatarini kukumbwa na janga la njaa.

Akijibu swali Mhe.Masanja amesema, "Tumekuwa tukifanya uthamini pale ambapo kumekuwa kunatokea changamoto ya tembo kuingia kwenye maeneo ya kilimo na tunapofanya utahamini tunawalipa wa fidia kulinganana uthamini ulivyofanyika, tunalipa fidia kulingana na athari ilivyojitokeza,"

Pia Mhe.Masanja  akielezea juu ya kiwango kinachotozwa cha shillingi laki moja pale ngombe moja atapoingia kwenye hifadhi amesema, "kuhusu namna ambavyo tunatoza ngome laki moja, tutambue sheria ni sisi wenyewe tumezitunga na sisi ni wataekelezaji wa sheria, Mhe.Spika  na hiki kiwango kipo kwenye sheria ya wanyama sio kwamba sisi tumekiamua,"