Vifaa tiba vilivyowasili nchini
Katika taarifa yake aliyoiandika kupitia ukurasa wake wa Twitter Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, amemshukuru mfanyabiashara huyo pamoja na Serikali ya China kwa ujumla.
"Jana usiku sisi Tanzania tulipokea mchango wa vifaa tiba, ambavyo vitasaidia katika mapambano yetu dhidi ya COVID-19, shukrani zetu za dhati kwa mfanyabiashara JackMa na taasisi yake ya AlibabaGroup na Serikali ya Ethiopia" Ameandika Waziri Ummy.
Vifaa hivyo ni barakoa 100,000, vipimo 20,000, na mavazi ya kujilinda (protective suits) 1,000.