Jumanne , 13th Feb , 2024

Serikali imesema kuwa imelipa jumla ya Shilingi trilioni 1.03 kati ya shilingi trilioni 1.41 za madeni ya wazabuni yaliyohakikiwa na Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali (IAG) na kukidhi vigezo ikiwa ni sawa na asilimia 73.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali bungeni jijini Dodoma la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Ritha Kabati alietaka kufahamu Serikali imewalipa wazabuni wangapi wanaozidai taasisi mbalimbali nchini na kiasi gani kimelipwa.

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Ritha Kabati alietaka kufahamu Serikali imewalipa wazabuni wangapi wanaozidai Taasisi mbalimbali nchini na kiasi gani kimelipwa.

Mhe. Chande alisema kuwa Idadi ya Wazabuni waliolipwa ni 8,830 ambao walikuwa wakidai Taasisi mbalimbali za Serikali. Ulipaji huo ni hatua ya Serikali katika kuchochea uchumi na kukuza sekta binafsi.

 Alisema kuwa Serikali inaendelea kuwalipa wazabuni kwa kadri fedha zitakavyopatikana na pia ulipaji ni lazima ufuate taratibu kwa kuwa suala la zabuni hutolewa kwa mkataba na ni suala la kisheria.