Mji wa Chinhoyi upo umbali wakilomita 115 kufikia mji mkuu wa nchi hiyo Harare.
Katika tamko lao walilolitoa kwenye ukurasa wao wa mtandao wa kijamii wa Twitter, Muungano huo umesema kwamba Kiongozi wao Nelson Chamisa alilengwa kushambuliwa na msafara wake kwa kutumia milipuko wakati akikaribia ukumbi mmoja wa mkutano mjini humo.
Taarifa ya CCC imeongeza kuwa Ukumbi huo pia ulilipuliwa na bomu la petrol jumamosi ya juzi yna watu wasiojulikana. Chama hicho kimepeleka lawama zake kwa wale iliyowaita vijana wa chama tawala nchini humo Zanu-PF kwa mashambulizi hayo. Serikali haijajibu lolote kuhusiana na madai hayo.
Shambulizi hilo limetokea ikiwa ni wiki kadhaa zimepita toka Bwana Chamisa ashambuliwe yeye na msafara wake na vijana wanaosaidikwa kuwa anatokea chama tawala. Joto la kisiasa lipandana nchini Zimbabwe kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.





