
Korosho
Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Mtwara Brigedia Jenerali Marco Gaguti, ametoa saa 48 kwa Mkurugenzi wa kampuni ya Makonde Sulfa inayodaiwa kusambaza pembejeo feki za zao la korosho kujisalimisha kwa jeshi la polisi mkoani humo.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa mkoa huo amesema mbali na kujisalimisha kwa mfanyabiashara huyo, ambae anadaiwa kuuza pembejeo zisizofa kwa wakulima, tayari mamlaka zinawashikilia watu saba wanaodaiwa kuhusika na sakata hilo.