
Maalim Seif, Edward Lowassa na Zitto Kabwe
Kesi hiyo Na. 112/2018 inatarajiwa kuanza kusomwa asubuhi hii huku Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe pamoja na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko wakitokea gereza la Segerea.
Viongozi ambao watahudhuria kesi hiyo ni, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT-wazalendo, Zitto Kabwe na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif.
Viongozi Wakuu wa CHADEMA wanaokabiliwa na kesi hiyo ni pamoja na M/kiti wa Chama Freeman Mbowe (Mb) KM Dkt Mashinji, NKMB Mnyika (Mb), NKMZ Salum Mwalim, Mkt wa BAWACHA Taifa Halima Mdee (Mb), John Heche (Mb), Ester Matiko (Mb) na Peter Msigwa (Mb).
Wanakabiliwa na kesi ya kula njama na kufanya mikusanyiko isiyokuwa ya halali iliyopelekea mwanafunzi wa chuo cha Usafirishaji NIT, Aqwiline Akwilini kupoteza maisha baada ya kupigwa risasi.