
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini Tanzania, Wilbroad Mutafungwa
Akiwa katika ziara yake mkoani Songwe, Kamanda Mutafungwa alikutana na madereva wa malori na It na kuwasisitizia madereva hao matumizi sahihi ya sheria na alama za barabarani.
"Wako baadhi ya wamiliki wa makampuni ambao wao ukimuambia gari haina tairi anakuambia lete dereva mwingine tuendelee na safari, wamiliki wa aina hiyo hakika wanakuwa wameshiriki kwa kiasi kikubwa kuangamiza watu tutakapogundua gari limebeba mzigo ni bovu tutamwajibisha dereva na tutatafuta jinsi ya kumwajibisha mmiliki", ameongeza Kamanda Mutafungwa.