Jumamosi , 25th Feb , 2023

Wanafunzi wanne wa shule ya Msingi Kagera iliyopo Mgumile kata ya Kagera manispaa ya Kigoma wanahofiwa kufa maji huku wanafunzi wawili wakiokolewa baada ya mtumbwi waliokuwa wakitumia kuvuka kwenye mto Luiche kwenda shule kupigwa na dhoruba na kupinduka

Mkuu wa wilaya Kigoma, Salum Kalli akitoa taarifa kwa waandishi a habari mjini Kigoma alisema kuwa kuzama kwa mtumbwi huo kunatokana na mto kujaa kulikosababishwa na mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia siku ya tukio

Mkuu huyo wa wilaya Kigoma alisema kuwa Nahodha wa mtumbwi huo Dunia Andrea (61)  kwa nafasi yake alijitahidi na kufanikiwa kuokoa watoto wawili ambao maji yalikuwa yakitembea kwa kasi kuelekea ziwa Tanganyika umbali wa kilometa tatu kutoka eneo la tukio.