Jumamosi , 25th Feb , 2023

Watu wawili  wamefariki dunia kwa ajali iliyotokea iliyotokea maeneo ya Nyololo Wilayani Mufindi ikihusisha kugongana kwa magari mawili ya mizigo

Watu hao ambao bado hawajafahamika kwa majina yao ni dereva mmoja na Mwanamke mmoja ambaye mwili wake umeungua na moto 

Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Dkt Linda Salekwa amefika eneo la ajali na kuwasihi madereva kuendelea kuwa waangalifu wakiwa barabarani

Miili ya marehemu hao imehifadhiwa kwenye Hospitali ya Mji wa Mafinga