Punda
Akimwakilisha Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mashimba Ndaki kwenye kongamano la kujadili ustawi wa punda Afrika, ambapo amesisitiza kuwa serikali ya Tanzania inaendelea kusimamia katazo la uchinjaji wa punda nchini.
Aidha Wizara ya Mifugo imeagizwa kutenga bajeti ya kuendeleza uzalishaji wa punda pamoja na kutoa elimu zaidi kuhusu fursa za ufugaji wa punda nchini.
Kwa upande wake Waziri wa Mifugo amebainisha kuwa Senegal wataendelea kufanya tafiti zitakazo kuja na suluhisho la kuongeza uzalishaji wa Punda Afrika.