Jumapili , 25th Apr , 2021

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Ummy Mwalimu amewasimamisha kazi wakurugenzi wawili wa Mamlaka za Serikali za mtaa kuanzia leo Aprili 25, 2021.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Ummy Mwalimu

Wakurugenzi hao ni Lusubilo Joel Mwakabibi wa Halmashauri ya  Manispaa ya Temeke na Nyangi John Msemakweli wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga.

Waziri Ummy amefikia uamuzi wa kumsimamisha kazi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke Lusubilo Mwakabibi, baada ya kupokea malalamiko juu ya mwenendo usiofaa, matumizi mabaya ya madaraka na mwenendo usioridhisha wa usimamizi wa miradi ya maendeleo.

Zaidi soma zaidi taarifa ya Wizara