Zitto Kabwe
Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu wa Uenezi wa chama hicho Ado Shaibu, imeeleza kuwa sbabu kubwa ya kushikiliwa ni haruhusiwi kusafiri kwenda nje ya Tanzania.
''ACT Wazalendo inawajulisha wanachama wake na Watanzania kuwa kiongozi wetu wa Chama ndugu Zitto Kabwe, ameshikiliwa na mamlaka za Serikali tangu saa nane mchana leo'', imeeleza taarifa hiyo.
Aidha Ado ameongeza kuwa kiongozi huyo ameshikiliwa na maofisa wa Uhamiaji Zanzibar kwa maelekezo kuwa haruhusiwi kusafiri kwenda nje ya nchi ambapo kiongozi huo alikuwa akisafiri kwenda nchini Kenya.