Ijumaa , 16th Apr , 2021

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai amesema suala la uaminifu linahitaji kujadiliwa kutokana na vijana watanzania kulalamikiwa kutokuwa waaminifu kwenye miradi mbalimbali.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai

Spika Ndugai amesema hayo leo, Bungeni mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na kusem kuwa  iko haja ya suala la uaminifu kujadiliwa na wabunge kwani kiwango cha uaminifu ni kidogo sana.

"Wawekezaji wengi wamekuwa wakilalamikia suala la uaminifu kwa vijana hasa vijana Tanzania uaminifu ni mdogo, katika miradi ndani ya sekta mbalimbali ukiwaweka unajikuta unafirisika eneo hili sijui dawa yake nini?," amesema Spika Ndugai

Pia Ndugai amesema iko haja ya viongozi wa dini , shule na wazazi wanapaswa kuwekeza nguvu ya ziada katika kufundisha na kuhubiri kuhusiana na uaminifu ili kujenga jamii yenye uaminifu.

"Iko haja ya Viongozi wetu wa dini wa madhehebu mbalimbali kuweza kuhubiri kuhusiana na uaminifu, shuleni mitaala, na wazazi tujenge jamii ambayo ni ya watu waaminifu wasio kuwa na tamaa, leo ukiwekeza afu uje bungeni umewaachia miezi sita ujawatemebelea utakuta umepigwa" amesema Ndugai