Jumamosi , 21st Jun , 2014

Tanzania R&B One, Ben Pol akiwa kama moja ya wasanii wa awali kabisa hapa Bongo, kuingiza muziki wake katika soko la kisasa la mtandao, amesema kuwa ana imani kuwa katika siku zijazo kibongo bongo soko la muziki litaweza kuchangamka zaidi

Ben Pol

Ben Pol amesema haya kutokana na ukweli kuwa kwa sasa mambo bado rekodi za mauzo haziridhishi kwa upande huo.

Ben Pol ambaye ni moja ya wakali wanaoshambulia Jukwaa katika Kili Tour kule Iringa katika Viwanja vya Samora, amesema kuwa bado wasanii wanahesabu faida ya ngoma wanazotoa kupitia shows, kitu ambacho kinaleta changamoto katika swala zima la rekodi ya faida ambayo wanakuwa wameingiza kupitia mauzo ya singo.

Ben Pol, kuhusuana na hili, hapa mwenyewe anasema.