Jumatatu , 10th Dec , 2018

Msanii wa Hip Hop nchini Marekani, Chance The Rapper ameamua kuacha kufanya muziki kwa muda na kwenda kujifunza biblia, ili aweze kumjua Mungu zaidi na kuwa mfano bora kwa mtoto wa dada yake.

Chance ameandika ujumbe akitoa taarifa ya uamuzi huo kwenye ukurasa wake wa instagram, ambapo ameeleza namna ambavyo alikulia kwenye familia ya kidini, na kujuta kwake kwa kutofuata misingi hiyo ya kumjua Mungu zaidi.

Hatua hiyo imekuja wiki moja baada ya kuachia audio ya ngoma yake mpya inayojulikana kwa jina la 'The man who has everything'.

 

I’m on a plane headed out the country on my first sabbatical. I’m going away to learn the Word of God which I am admittedly very unfamiliar with. I’ve been brought up by my family to know Christ but I haven’t taken it upon myself to really just take a couple days and read my bible. we all quote scripture and tell each other what God likes and doesn’t like but how much time do we spend as followers of Jesus to really just read and KNOW his Word. I’m definitely guilty of not devoting time to it. So I’m off to read and learn because the next generation of Bennett is here and I need to be able to give my nephew Charlie Matthew the knowledge and tools to FUCK YALL UP. Lol but seriously he’s the first boy of the next line and he needs his uncle to be educated. So dont bother me, ill be back soon enough, with five or more books from bible read. Oh yeah and cigarette free 

A post shared by Chance The Rapper (@chancetherapper) on

Hivi karibuni msanii huyo alitajwa kuwa na uhusiano na msanii mwenzake wa kiume, Jaden Smith, ambapo inadaiwa wawili hao walikuwa na uhusiano kwa kipindi kirefu lakini walikuwa wakifanya kwa siri.