Kushoto ni Country Boy na kulia ni Lil Wayne
Country Boy amesema anapenda sana kuvaa, kwenda na fashion ila anawatumia mastaa wakubwa kama Lil Wayne, Wiz Khalifa na Migos ila sio kama anawaiga kila kitu na kuzidisha uhalisia wake.
"Ni katika aina ya kujikubali na kujipenda nimekuwa nafatilia vitu vingi na napenda "fashion" na kuangalia ubunifu wa watu wanavyovaa. Mimi navaa tofauti na watu wengi sana, huwa navaa vitu vinavyoitwa nyuki lazima vionekane. Watu ninaowafuatilia ni wanyamwezi sana kama Lil Wayne, Wiz Khalifa na Migos" ameeleza
Aidha akizungumzia kuhusu watu na mashabiki kumsema kuwa anamuiga Lil Wayne hadi kupitiliza uhalisia wake Country Boy amesema
"Nadhani aliyesema hivo alikuwa na mawazo ya kimaisha na akaamua kusema hivyo maani mimi najiona nimejipata katika uhalisia wangu labda wameniona pengine nina rasta, Lil Wayne anatumia "Auto tunes" mimi natumia sauti nyingine kabisa . Mashabiki wanataka wakutoe kwenye njia ili umjibu" ameongeza.



