
Mashindano ya kucheza muziki ya Dance100% 2014
Mashindano haya yatakayohusisha makundi 16 makali ya kudansi, yatafanyika kesho Jumamosi katika uwanja wa Oysterbay Don Bosco, na makundi yataanza kuonesha uwezo mbele ya majaji kuanzia saa 6 mchana.
Tukio hili linatarajiwa kuwa na msisimko wa aina yake hasa kutokana na ushindani na uwezo mkubwa wa makundi yote ambayo yanashiriki. Dance100% 2014 yanakwenda na swagga ya #2014Dance100%.
Tukutane Jumamosi hapo kesho katika uwanja wa Oysterbay Don Bosco jijini Dar es Salaam.
