Msanii wa BongoFleva Ditto
Akifafanua hilo kwenye kipindi cha MamaMia ya East Africa Radio, msanii Ditto amesema kuwa yeye kama mwanaume anaelewa nini kinakachofuata au kitakachotokea mwisho wa urafiki huo.
"Ndani ya urafiki wa mwanaume na mwanamke lazima kuna Jambo limejificha sijawahi kuona na kama wapo marafiki basi ni mmoja duniani tusidanganyane mimi ni mwanaume naelewa wanaume hatuwezi labda wanawake wanaweza vumilia urafiki ila sisi wanaume hatuwezi" amesema Ditto
Aidha Ditto ameendelea kusema "Mwanaume lijali lazima apate hisia hata kama mtakuwa ni marafiki, kuna muda hisia zinakuja asikudanganye mtu urafiki wa jinsia mbili haupo"