Jumapili , 3rd Jan , 2021

Msanii wa Bongofleva ambaye hivi sasa anatamba na ngoma yake ya Wapo, Harmonize, amerejea nchini leo Januari 3, 2021 akitokea Ghana na moja kwa moja akaahidi kuwa usiku wa leo atarekodi ngoma yake ya kwanza mwaka huu akimshirikisha mwimbaji Abella.

Harmonize (kulia) na Abella (kushoto)

Harmonize akiwa nje ya nchi jana Januari 2, 2021, alitangaza kutafuta mwimbaji wa kike ili amshirikishe kwenye ngoma yake hiyo na baada ya mapendekezo ya watu alitangaza kumtafuta mwimbaji wa nyimbo za kurudia 'Cover', aitwaye Abella na alifanikiwa kumpata.

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

A post shared by KONDEBOY (@harmonize_tz)

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

A post shared by KONDEBOY (@harmonize_tz)

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Harmonize amethibitsha kuwa amerejea nchini leo na usiku anakutana na Abella kwaajili ya kurekodi audio ya wimbo huo.

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

A post shared by KONDEBOY (@harmonize_tz)

Abella ambaye ana ulemavu wa mguu amejizolea umaarufu mtandaoni kwa kurudia nyimbo za wasanii mbalimbali huku wengi wakisifia uwezo wake mkubwa pamoja na sauti ya kuvutia.