Kutoka upande wa kushoto ni Harmonize, kulia Ibraah Tz
Ibraah Tz amesema anamshukuru Harmonize kwa sababu, alimkuta hayupo vizuri na bila ya kuwa na kipaji cha kutosheleza lakini akatengenezwa hadi amefikia alipo sasa.
"Kabla ya hapo nilikuwa naendaga sana getini kwake kuomba nafasi ya kuonana naye na nikafanya hivyo kwa miezi miwili lakini sikupata nafasi hiyo, ila kuna mjomba wangu alikuwa ananisadia kunipa nauli, akajitahidi kunikutanisha na producer Bonga ndiyo nikapata nafasi ya kufika Konde Music" ameeleza Ibraah Tz
Pia Ibraah Tz ameendelea kusema kabla hajasainiwa Konde Music, ameshazunguka sana kwenye studio na wasanii wengine kutafuta msaada ila ikashindikana japo hawezi kuwazungumzia kwa sasa wasanii hao ni kina nani.