Moja kati ya nyumba zilizowaka moto nchini Marekani kati mji wa California
Kupitia ukurasa wa Twitter wa Kanye West ameandika “Najenga jamii ya kuzuia moto kushika”.
Building a fireproof community
— ye (@kanyewest) November 16, 2018
Rapper Kanye West pamoja na mke wake Kim Kardashian waliajiri watu maalum wa uzimaji moto kwaajili ya kuzima moto uliosababisha uharibifu mkubwa wa nyumba za watu zaidi ya 27000 na maelfu ya watu kupotea.
Moto huo mkubwa ulizuka na kuteketeza baadhi ya nyumba kwenye makazi ya kifahari ya Hidden Hills mjini California ikiwemo na nyumba nyingine kuteketea kabisa na kusababisha vifo vya watu 71 mpaka sasa wakiwemo watu wa zima moto na kundi kubwa la watu kujikuta wakikosa makazi ya kuishi.