Jumapili , 18th Nov , 2018

Rapper Kanye West ‘Ye’ amekuja na mpango wa kujenga nyumba ambayo haitashika moto, baada ya tukio la nyumba yake yenye thamani zaidi ya shillingi Billioni 100 za Kitanzania kuwa miongoni mwa nyumba zilizoungua moto siku kadhaa zilizopita  Mjini California Marekani.

Moja kati ya nyumba zilizowaka moto nchini Marekani kati mji wa California

Kupitia ukurasa wa Twitter wa Kanye West ameandika “Najenga jamii ya kuzuia moto kushika”.

Rapper Kanye West pamoja na mke wake Kim Kardashian waliajiri watu maalum wa uzimaji moto kwaajili ya kuzima moto uliosababisha uharibifu mkubwa wa nyumba za watu zaidi ya 27000 na maelfu ya watu kupotea.

Moto huo mkubwa ulizuka na kuteketeza baadhi ya nyumba kwenye makazi ya kifahari ya Hidden Hills mjini California ikiwemo na nyumba nyingine kuteketea kabisa na  kusababisha vifo vya watu 71 mpaka sasa wakiwemo watu wa zima moto na kundi kubwa la watu kujikuta wakikosa makazi ya kuishi.