Upande wa kushoto Petitman Wakuache na Wema Sepetu , kulia ni Kajala Masanja
Petitman Wakuache amesema tatizo la Wema Sepetu na Kajala Masanja linazungumziwa kwa sasa ila bado hajakaa kuzungumza nao ila kuna umuhimu wa kusameheana kwa sababu maisha ni mafupi pia kuna kifo.
"Kuhusu suala la Wema na Kajala lipo-trending kwa sasa ukizingatia kauli ya Wema Sepetu aliyoisema, kwa upande wangu huo mchakato wa kuwapatanisha unafanyika na nina mipango hiyo ya kumaliza toafuti zao, wale ni marafiki waliokuwa nusu ndugu, matatizo yanatokea kwa binadamu na tunakoseana ila mwisho wa siku tunapatana, maisha yenyewe mafupi sana kuna kifo pia" ameeleza Petitman Wakuache