Ijumaa , 22nd Aug , 2014

Malkia wa Mipasho, Khadija Kopa ameweka wazi kuwa ameamua sasa kufanya kazi ya nguvu pamoja na watoto wake kupitia kundi ambalo amalelitengeneza linalokwenda kwa jina "Ogopa Kopas".

msanii wa Mipasho Khadija Kopa akiwa na wanawe

Malkia huyo gwiji wa miondoko hiyo nchini amesema kundi hilo jipya litaufikisha muziki wa Taarab hapa Bongo katika ngazi nyingine ya juu kabisa.

Khadija ameiambia eNewz kuwa, akiwa kama msanii msomi, kundi lake la Ogopa Kopaz litaanza kazi kwa kasi likitanguliwa na ujio wa albam zake mbili 'Mama Mukubwa' na 'Kantangaze'.